Zaburi 124

Zaburi 124

Shukrani kwa ukombozi wa Israeli

1Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi,[#Mwa 15:1; Hes 14:9; Yos 1:5; Ebr 13:5; Rum 8:31]

Israeli na aseme sasa,

2Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi,

Wanadamu walipotushambulia.

3Papo hapo wangalitumeza hai,[#Zab 35:25; Mit 1:12; Yer 51:34]

Hasira yao ilipowaka juu yetu.

4Papo hapo maji yangalitugharikisha,

Mto ungalipita juu ya roho zetu;

5Papo hapo maji yafurikayo

Yangalipita juu yetu.

6Na ahimidiwe BWANA;

Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao.

7Nafsi yetu imeokoka kama ndege

Katika mtego wa wawindaji,

Mtego umevunjika, nasi tumeokoka.

8Msaada wetu u katika jina la BWANA,[#Kut 18:4; Zab 12:2; Mit 18:10; Isa 50:10; Ebr 13:6]

Aliyeziumba mbingu na nchi.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya