Zaburi 129

Zaburi 129

Sala ya kushindwa kwa adui za Israeli

1Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu,[#Eze 23:3; Hos 2:15]

Israeli na aseme sasa,

2Mara nyingi wamenitesa tangu ujana wangu,

Lakini hawakuniweza.

3Wakulima wamelima mgongoni mwangu,[#Ebr 11:36]

Wamefanya mirefu mifuo yao.

4BWANA ndiye mwenye haki,[#2 The 1:6]

Amezikata kamba zao wasio haki.

5Na waaibishwe, warudishwe nyuma,

Wote wanaoichukia Sayuni.

6Na wawe kama majani ya darini[#Zab 37:2; Yer 17:5-6]

Yanyaukayo kabla hayajamea.

7Ambayo mvunaji haujazi mkono wake,

Wala mfunga miganda kifua chake.

8Wapitao nao hawasemi, Amani ya BWANA ikae nanyi,[#Rut 2:4; Zab 118:26]

Twawabariki kwa jina la BWANA.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya