Zaburi 131

Zaburi 131

Kumtumainia Mungu kwa utulivu

1BWANA, moyo wangu hauna kiburi,[#Rum 12:16]

Wala macho yangu hayainuki.

Wala sijishughulishi na mambo makuu,

Wala mambo yanayozidi nguvu zangu.

2Hakika nimeituliza nafsi yangu,[#Mt 18:3]

Na kuinyamazisha.

Kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

Kifuani mwa mama yake;

Roho yangu ni kama mtoto,

Aliyeachishwa kunyonya.

3Ee Israeli, umtarajie BWANA,

Tangu leo na hata milele.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya