The chat will start when you send the first message.
1Kwa sauti yangu nitamlilia BWANA,[#1 Sam 22:1; 24:3]
Kwa sauti yangu nitamwomba BWANA dua.
2Nitafunua mbele zake malalamiko yangu,
Shida yangu nitaitangaza mbele zake.
3Roho yangu inapozimia unayajua mapito yangu;
Katika njia niendayo wamenifichia mtego.
4Utazame mkono wangu wa kulia ukaone,
Kwa maana sina mtu anijuaye.
Makimbilio yamenipotea,
Hakuna wa kunitunza roho.
5BWANA, nimekuita nikasema, Ndiwe kimbilio langu,[#Omb 3:24]
Fungu langu katika nchi ya walio hai.
6Ukisikilize kilio changu,[#Zab 116:6; 7:1]
Kwa maana nimedhilika sana.
Uniponye kutoka kwa wanaonifuatia,
Kwa maana wao ni hodari kuliko mimi.
7Uitoe nafsi yangu kifungoni.[#Zab 34:2; 119:17]
Nipate kulishukuru jina lako.
Wenye haki watanizunguka,
Kwa kuwa Wewe unanikirimu.