The chat will start when you send the first message.
1Haleluya.[#146:1 maana yake ni, Msifuni BWANA.]
Ee nafsi yangu, umsifu BWANA.
2Nitamsifu BWANA muda ninaoishi,
Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.
3Msiwatumainie wakuu,[#Isa 2:22]
Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.
4Pumzi yake inapomtoka, anarudi katika udongo wake,[#Mhu 12:7; 1 Kor 2:6]
Siku iyo hiyo mipango yake hutoweka.
5Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,[#Yer 17:7]
Na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake,
6Aliyezifanya mbingu na nchi,[#Mik 7:20; Mdo 4:24; 14:15; Ufu 14:7]
Bahari na vitu vyote vilivyomo.
Huishika kweli milele,
7Huwafanyia hukumu walioonewa,
Huwapa wenye njaa chakula;
BWANA hufungua waliofungwa;
8BWANA huwafumbua macho waliopofuka;
BWANA huwainua walioinama;
BWANA huwapenda wenye haki;
9BWANA huwahifadhi wageni;
Huwategemeza yatima na mjane;
Bali njia ya wasio haki huiharibu.
10BWANA atamiliki milele,
Mungu wako, Ee Sayuni, kwa vizazi vyote.
Haleluya.