Zaburi 3

Zaburi 3

Mwamini Mungu katika dhiki

1BWANA, watesi wangu wamezidi kuwa wengi,[#2 Sam 15:13—17:22]

Ni wengi wanaonishambulia,

2Ni wengi wanaoiambia nafsi yangu,[#2 Sam 16:8; Zab 22:7,8]

Hana wokovu huyu kwa Mungu.

3Lakini Wewe, BWANA, U ngao yangu pande zote,[#2 Fal 25:27; Zab 27:6]

Utukufu wangu na mwinua kichwa changu.

4Kwa sauti yangu namwita BWANA

Naye aniitikia toka mlima wake mtakatifu.

5Nilijilaza na kulala usingizi, kisha ninaamka tena,[#Zab 4:8; Mit 3:24; Mdo 12:6]

Kwa kuwa BWANA ananitegemeza.

6Sitayaogopa maelfu na maelfu ya watu,

Waliojipanga Juu yangu pande zote.

7BWANA, uinuke, Mungu wangu, uniokoe,

Maana umewapiga taya adui zangu wote;

Umewavunja meno wasio haki.

8Wokovu ni wa BWANA;[#Zab 37:39,40; Mit 21:31; Hes 13:4]

Baraka yako na iwe juu ya watu wako.

Swahili Revised Union Version Bible © Bible Society of Kenya, and Bible Society of Tanzania, 2005.
Published by: Bible Society of Kenya