The chat will start when you send the first message.
1Ni kweli, enyi wakuu, mnanena haki?
Enyi wanadamu, mnahukumu kwa adili?
2Sivyo! Mioyoni mwenu mnatenda maovu;[#Zab 94:20]
Mikono yenu wenyewe inaeneza udhalimu katika nchi.
3Waovu hupotoka hata kabla ya kuzaliwa kwao;[#Zab 51:5]
Tangu tumboni wamepotea, wakisema uongo.
4Wana sumu mfano wa sumu ya nyoka;[#Zab 140:4]
Wao ni kama fira kiziwi azibaye sikio lake.
5Asiyeisikiliza sauti ya waganga,
Ijapo wanafanya uganga kwa ustadi.
6Ee Mungu, uyavunje meno yao vinywani mwao;[#Ayu 4:10]
Ee BWANA, uyavunje magego ya wanasimba.
7Na watoweke kama maji yapitayo kwa kasi;
Akiielekeza mishale yake, iwe imetiwa ubutu.
8Kama konokono ayeyukaye na kutoweka,
Kama mimba iliyoharibika, isiyoliona jua,
9Kabla ya masufuria yenu kupata moto wa miiba,[#Mit 10:25]
Ataipeperusha kama chamchela,
Iliyo mibichi na iliyo moto.
10Mwenye haki atafurahi akionapo kisasi;[#Kum 32:42; Ayu 22:19; Zab 18:47; Mit 10:11; Ufu 18:20]
Ataiosha miguu yake katika damu ya wasio haki.
11Na mwanadamu atasema,[#Rum 2:6-11; Ayu 34:11; Mhu 5:8; Yer 32:19; Eze 7:27; Rum 14:12; Ufu 2:23]
Hakika iko thawabu yake mwenye haki.
Hakika yuko Mungu
Anayehukumu katika dunia.