The chat will start when you send the first message.
1Ee MUNGU, Mungu wangu, nitakutafuta mapema,[#1 Sam 23:14]
Nafsi yangu inakuonea kiu,
Mwili wangu wakuonea shauku,
Katika nchi kame na uchovu, isiyo na maji.
2Ndivyo nilivyokutazama katika patakatifu,[#1 Nya 16:11]
Nizione nguvu zako na utukufu wako.
3Maana fadhili zako ni njema kuliko uhai;[#Yn 3:16]
Midomo yangu itakusifu.
4Ndivyo nitakavyokubariki maadamu ni hai;
Kwa jina lako nitaiinua mikono yangu.
5Nafsi yangu itakinai kama kushiba mafuta na vinono;[#Zab 17:15; Isa 25:6]
Kinywa changu kitakusifu kwa midomo ya furaha.
6Ninapokukumbuka kitandani mwangu,[#Zab 149:5]
Ninakutafakari usiku kucha.
7Maana Wewe umekuwa msaada wangu,[#2 Kor 1:10]
Na uvulini mwa mbawa zako nitashangilia.
8Nafsi yangu inaambatana nawe sana;[#Isa 26:9]
Mkono wako wa kulia unanitegemeza.
9Bali waitafutao nafsi yangu, ili kuiangamiza,
Wataingia katika vilindi vya nchi.
10Watatolewa wafe kwa nguvu za upanga,
Watakuwa riziki za mbwamwitu.
11Bali mfalme atamfurahia Mungu,[#Sef 1:5]
Kila aapaye kwa Yeye atashangilia,
Kwa maana vinywa vya waongo vitafumbwa.