1 Tim 3

1 Tim 3

Sifa za Maaskofu

1Ni neno la kuaminiwa; mtu akitaka kazi ya askofu, atamani kazi njema.[#Mdo 20:28; #3:1 maana yake ni, Mwangalizi.]

2Basi imempasa askofu awe mtu asiyelaumika, mume wa mke mmoja, mwenye kiasi na busara, mtu wa utaratibu, mkaribishaji, ajuaye kufundisha;[#Tit 1:6-9]

3si mtu wa kuzoelea ulevi, si mpiga watu; bali awe mpole; si mtu wa kujadiliana, wala asiwe mwenye kupenda fedha;

4mwenye kuisimamia nyumba yake vema, ajuaye kutiisha watoto katika ustahivu;[#1 Sam 2:12]

5(yaani, mtu asiyejua kuisimamia nyumba yake mwenyewe, atalitunzaje Kanisa la Mungu?)

6Wala asiwe mtu aliyeongoka karibu, asije akajivuna akaanguka katika hukumu ya Ibilisi.

7Tena imempasa kushuhudiwa mema na watu walio nje; ili asianguke katika lawama na mtego wa Ibilisi.[#1 Tim 5:10; 2 Kor 8:21; 1 Kor 5:12,13]

Sifa za Mashemasi

8Vivyo hivyo mashemasi8 na wawe wastahivu; si wenye kauli mbili, si watu wa kutumia mvinyo sana, si watu wanaotamani fedha ya aibu;[#Flp 1:1; Mdo 6:3; #3:8 maana yake ni, Mtumishi wa Kanisa.]

9wakiishika siri ya imani katika dhamiri safi.

10Hawa pia na wajaribiwe kwanza; baadaye waitende kazi ya shemasi, wakiisha kuonekana kuwa hawana hatia.

11Vivyo hivyo wake zao na wawe wastahivu; si wasingiziaji; watu wa kiasi, waaminifu katika mambo yote.[#Tit 2:3]

12Mashemasi na wawe waume wa mke mmoja, wakiwasimamia watoto wao vizuri, na nyumba zao.

13Kwa maana watendao vema kazi ya shemasi hujipatia daraja nzuri, na ujasiri mwingi katika imani iliyo katika Kristo Yesu.

Siri ya Dini Yetu

14Nakuandikia hayo nikitaraji kuja kwako hivi karibu.

15Lakini nikikawia, upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa kweli.[#2 Tim 2:20; Efe 2:19-22]

16Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu.[#Yn 1:14; 16:10; Rum 1:4; Mk 16:19]

Mungu alidhihirishwa katika mwili,

Akajulika kuwa na haki katika roho,

Akaonekana na malaika,

Akahubiriwa katika mataifa,

Akaaminiwa katika ulimwengu,

Akachukuliwa juu katika utukufu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania