The chat will start when you send the first message.
1Mimi ndimi mzabibu wa kweli, na Baba yangu ndiye mkulima.[#Yer 2:21; Zab 80:8]
2Kila tawi ndani yangu lisilozaa huliondoa; na kila tawi lizaalo hulisafisha, ili lizidi kuzaa.[#Mt 15:13]
3Ninyi mmekwisha kuwa safi kwa sababu ya lile neno nililowaambia.
4Kaeni ndani yangu, nami ndani yenu. Kama vile tawi lisivyoweza kuzaa peke yake, lisipokaa ndani ya mzabibu; kadhalika nanyi, msipokaa ndani yangu.
5Mimi ni mzabibu; ninyi ni matawi, akaaye ndani yangu nami ndani yake, huyo huzaa sana; maana pasipo mimi ninyi hamwezi kufanya neno lo lote.[#1 Kor 12:12,27; 2 Kor 3:5]
6Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatupa motoni yakateketea.[#Mt 3:10; 13:40]
7Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.[#Mk 11:24]
8Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.[#Mt 5:16]
9Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu.
10Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.[#Yn 8:29; 14:15; 1 Yoh 2:4,8]
11Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.[#Yn 17:13]
12Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.[#Yn 13:34; 15:17; 1 Yoh 3:11,23; 2 Yoh 1:5; Mk 12:30]
13Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.[#Yn 10:12; 1 Yoh 3:16]
14Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.[#Yn 8:31; Mt 12:50; 28:20]
15Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.
16Si ninyi mlionichagua mimi, bali ni mimi niliyewachagua ninyi; nami nikawaweka mwende mkazae matunda; na matunda yenu yapate kukaa; ili kwamba lo lote mmwombalo Baba kwa jina langu awapeni.[#Yn 6:70; 13:18]
17Haya nawaamuru ninyi, mpate kupendana.
18Iwapo ulimwengu ukiwachukia, mwajua ya kuwa umenichukia mimi kabla ya kuwachukia ninyi.[#Yn 7:7; 1 Yoh 3:13]
19Kama mngekuwa wa ulimwengu, ulimwengu ungewapenda walio wake; lakini kwa kuwa ninyi si wa ulimwengu, bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.[#1 Yoh 4:5; Yn 17:14; Lk 6:22]
20Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi; ikiwa walilishika neno langu watalishika na lenu.[#Mt 10:24; Lk 6:40; Yn 13:16]
21Lakini haya yote watawatenda kwa ajili ya jina langu, kwa kuwa hawamjui yeye aliyenipeleka.[#Yn 10:22; 16:3; Mt 5:11; Mk 13:13]
22Kama nisingalikuja na kusema nao, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa hawana udhuru kwa dhambi yao.
23Yeye anichukiaye mimi humchukia na Baba yangu.[#Yn 5:23; 1 Yoh 2:23; Lk 10:16]
24Kama nisingalitenda kwao kazi asizozitenda mtu mwingine, wasingalikuwa na dhambi; lakini sasa wametuona mimi na Baba yangu, na kutuchukia.[#Yn 14:11]
25Lakini litimie lile neno lililoandikwa katika torati yao, Walinichukia bure.[#Zab 35:19; 69:4]
26Lakini ajapo huyo Msaidizi, nitakayewapelekea kutoka kwa Baba, huyo Roho wa kweli atokaye kwa Baba, yeye atanishuhudia.[#Yn 14:26; Lk 24:49]
27Nanyi pia mnashuhudia, kwa kuwa tangu mwanzo mmekuwapo pamoja nami.[#Lk 1:2; Mdo 1:8; 5:32]