Ayu 17

Ayu 17

Ayubu Aomba Apate Faraja

1Roho yangu imezimika, siku zangu zimekoma,[#Zab 88:3,4]

Kaburi i tayari kunipokea.

2Ni kweli wako kwangu wenye kufanya dhihaka,[#1 Sam 1:6]

Jicho langu hukaa katika kunifanyia uchungu kwao.

3Nipe rehani basi, uwe dhamana kwa ajili yangu kwako wewe mwenyewe;[#Mit 6:1]

Kuna nani atakayeniwekea dhamana?

4Kwani mioyo yao imeificha ufahamu;

Kwa hiyo hutawakuza.

5Awafitiniye rafiki zake wawe mawindo,

Hata macho ya watoto wake yataingia kiwi.

6Amenifanya niwe simo kwa watu;[#1 Fal 9:7]

Nimekuwa mwenye kuchukiwa kwa wazi.

7Jicho langu nalo limekuwa giza kwa sababu ya majonzi,

Na via vyangu vyote vimekuwa kama kivuli.

8Walekevu watayastaajabia hayo,

Na asiye na hatia atajiamsha juu ya mpotovu.

9Lakini mwenye haki ataishika njia yake,[#Mit 4:18; Zab 24:4]

Naye mwenye mikono safi atazidi kupata nguvu.

10Lakini rudini; ninyi nyote, njoni sasa;[#Ayu 6:29]

Wala sitampata mtu mwenye hekima kati yenu.

11Siku zangu zimepita, makusudi yangu yamevunjika,[#Ayu 7:6; Isa 38:10]

Hata hayo niliyo nayo moyoni mwangu.

12Wabadili usiku kuwa mchana;

Wasema, Mwanga u karibu kwa sababu ya giza.

13Nikitazamia kuzimu kuwa nyumba yangu;

Nikitandika malazi yangu gizani;

14Ikiwa nimeuita uharibifu, Wewe u baba yangu;

Na kuliambia buu, Wewe u mama yangu, na umbu langu;

15Basi, tumaini langu li wapi?

Na tumaini langu, ni nani atakayeliona?

16Litashuka kwenye makomeo ya kuzimu,[#2 Kor 1:9; Zab 88:4-8; Ayu 3:17]

Itakapokuwapo raha mavumbini.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania