Zab 112

Zab 112

Baraka za Mwenye Haki

1Haleluya.

Heri mtu yule amchaye BWANA,

Apendezwaye sana na maagizo yake.

2Wazao wake watakuwa hodari duniani;

Kizazi cha wenye adili kitabarikiwa.

3Nyumbani mwake mna utajiri na mali,[#Mit 3:16; 15:6; Isa 33:6; Mt 6:33; 2 Kor 6:10]

Na haki yake yakaa milele.

4Nuru huwazukia wenye adili gizani;

Ana fadhili na huruma na haki.

5Heri atendaye fadhili na kukopesha;[#Lk 6:35]

Atengenezaye mambo yake kwa haki.

6Kwa maana hataondoshwa kamwe;

Mwenye haki atakumbukwa milele.

7Hataogopa habari mbaya;

Moyo wake u imara ukimtumaini BWANA.

8Moyo wake umethibitika hataogopa,

Hata awaone watesi wake wameshindwa.

9Amekirimu, na kuwapa maskini,[#Lk 11:41; Rum 12:13; Mdo 4:35; 20:35; 2 Kor 8:9; 9:9; 1 Tim 6:18]

Haki yake yakaa milele,

Pembe yake itatukuzwa kwa utukufu.

10Asiye haki ataona na kusikitika,[#Lk 13:28]

Atasaga meno yake na kuyeyuka,

Tamaa ya wasio haki itapotea.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania