Zab 120

Zab 120

Sala ya Ukombozi

1Katika shida yangu nalimlilia BWANA

Naye akaniitikia.

2Ee BWANA, uiponye nafsi yangu

Na midomo ya uongo na ulimi wa hila.

3Akupe nini, akuzidishie nini,

Ewe ulimi wenye hila?

4Mishale ya mtu hodari iliyochongoka,

Pamoja na makaa ya mretemu.

5Ole wangu mimi![#Mwa 10:2; 1 Sam 25:1; Yer 49:28]

Kwa kuwa nimekaa katika Mesheki;

Na kufanya maskani yangu

Katikati ya hema za Kedari.

6Nafsi yangu imekaa siku nyingi,

Pamoja naye aichukiaye amani.

7Mimi ni wa amani;

Bali ninenapo, wao huelekea vita.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania