Zab 121

Zab 121

Hakikisho la Ulinzi wa Mungu

1Nitayainua macho yangu niitazame milima,

Msaada wangu utatoka wapi?

2Msaada wangu u katika BWANA,

Aliyezifanya mbingu na nchi.

3Asiuache mguu wako usogezwe;[#1 Sam 2:9; Isa 27:3]

Asisinzie akulindaye;

4Naam, hatasinzia wala hatalala usingizi,

Yeye aliye mlinzi wa Israeli.

5BWANA ndiye mlinzi wako;

BWANA ni uvuli mkono wako wa kuume.

6Jua halitakupiga mchana,[#Isa 49:10]

Wala mwezi wakati wa usiku.

7BWANA atakulinda na mabaya yote,[#Ayu 5:19; Zab 91:9,10; Mit 12:21]

Atakulinda nafsi yako.

8BWANA atakulinda utokapo na uingiapo,[#Kum 28:6; Mit 2:8]

Tangu sasa na hata milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania