Zab 123

Zab 123

Ombi la Huruma

1Nimekuinulia macho yangu,

Wewe uketiye mbinguni.

2Kama vile macho ya watumishi

Kwa mkono wa bwana zao

Kama macho ya mjakazi

Kwa mkono wa bibi yake;

Hivyo macho yetu humwelekea BWANA, Mungu wetu,

Hata atakapoturehemu.

3Uturehemu, Ee BWANA, uturehemu sisi,

Kwa maana tumeshiba dharau.

4Nafsi zetu zimeshiba mzaha wa wenye raha,

Na dharau ya wenye kiburi.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania