Zab 124

Zab 124

Shukrani kwa Ukombozi wa Israeli

1Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi,[#Mwa 15:1; Hes 14:9; Yos 1:5; Ebr 13:5; Rum 8:31]

Israeli na aseme sasa,

2Kama si BWANA aliyekuwa pamoja nasi,

Wanadamu walipotushambulia.

3Papo hapo wangalitumeza hai,[#Zab 35:25; Mit 1:12; Yer 51:34]

Hasira yao ilipowaka juu yetu

4Papo hapo maji yangalitugharikisha,

Mto ungalipita juu ya roho zetu;

5Papo hapo yangalipita juu ya nafsi zetu

Maji yafurikayo.

6Na ahimidiwe BWANA;

Asiyetutoa kuwa mawindo kwa meno yao.

7Nafsi yetu imeokoka kama ndege

Katika mtego wa wawindaji,

Mtego umevunjika, nasi tumeokoka.

8Msaada wetu u katika jina la BWANA,[#Kut 18:4; Zab 12:2; Mit 18:10; Isa 50:10; Ebr 13:6]

Aliyezifanya mbingu na nchi.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania