The chat will start when you send the first message.
1Wamtumainio BWANA ni kama mlima Sayuni,
Ambao hautatikisika, wakaa milele.
2Kama milima inavyouzunguka Yerusalemu,
Ndivyo BWANA anavyowazunguka watu wake,
Tangu sasa na hata milele.
3Kwa maana fimbo ya udhalimu
Haitakaa juu ya fungu la wenye haki;
Wenye haki wasije wakainyosha
Mikono yao kwenye upotovu.
4Ee BWANA, uwatendee mema walio wema,
Nao walio wanyofu wa moyo.
5Bali wao wanaozigeukia njia zao zilizopotoka,[#Mit 2:15; Isa 59:8; Flp 2:15; Gal 6:16]
BWANA atawaondoa pamoja na watenda maovu.
Amani ikae na Israeli.