Zab 127

Zab 127

Baraka za Mungu Nyumbani

1BWANA asipoijenga nyumba

Waijengao wafanya kazi bure.

BWANA asipoulinda mji

Yeye aulindaye akesha bure.

2Kazi yenu ni bure, mnaoamka mapema,[#Mwa 3:17]

Na kukawia kwenda kulala,

Na kula chakula cha taabu;

Yeye humpa mpenzi wake usingizi.

3Tazama, wana ndio urithi wa BWANA,[#Mwa 33:5; Kum 28:4]

Uzao wa tumbo ni thawabu.

4Kama mishale mkononi mwa shujaa,

Ndivyo walivyo wana wa ujanani.

5Heri mtu yule

Aliyelijaza podo lake hivyo.

Naam, hawataona aibu

Wanaposema na adui langoni.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania