Zab 128

Zab 128

Nyumba ya Mwumini yenye Furaha

1Heri kila mtu amchaye BWANA,

Aendaye katika njia yake.

2Taabu ya mikono yako hakika utaila;[#Isa 3:10]

Utakuwa heri, na kwako kwema.

3Mkeo atakuwa kama mzabibu uzaao,

Vyumbani mwa nyumba yako.

Wanao kama miche ya mizeituni

Wakiizunguka meza yako.

4Tazama, atabarikiwa hivyo, yule amchaye BWANA.

5BWANA akubariki toka Sayuni;[#Zab 134:3]

Uone uheri wa Yerusalemu siku zote za maisha yako;

6Naam, ukawaone wana wa wanao.[#Mwa 50:23]

Amani ikae na Israeli.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania