Zab 131

Zab 131

Kumtumainia Mungu kwa Utulivu

1BWANA, moyo wangu hauna kiburi,[#Rum 12:16]

Wala macho yangu hayainuki.

Wala sijishughulishi na mambo makuu,

Wala na mambo yashindayo nguvu zangu.

2Hakika nimeituliza nafsi yangu,[#Mt 18:3]

Na kuinyamazisha.

Kama mtoto aliyeachishwa

Kifuani mwa mama yake;

Kama mtoto aliyeachishwa,

Ndivyo roho yangu ilivyo kwangu.

3Ee Israeli, umtarajie BWANA,

Tangu leo na hata milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania