Zab 133

Zab 133

Baraka za kuwa na Umoja

1Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza,[#Mwa 13:8; 1 Kor 1:10]

Ndugu wakae pamoja, kwa umoja.

2Ni kama mafuta mazuri kichwani,[#Kut 30:25]

Yashukayo ndevuni, ndevu za Haruni,

Yashukayo mpaka upindo wa mavazi yake.

3Kama umande wa Hermoni ushukao milimani pa Sayuni.[#Kum 4:48; 28:8; Law 25:11; Dan 12:2,3; Mt 25:34,46; Yn 4:14; 17:3; Ebr 7:25; 1 Yoh 5:20]

Maana ndiko BWANA alikoamuru baraka,

Naam, uzima hata milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania