Zab 134

Zab 134

Sifa ya Usiku

1Tazama, enyi watumishi wa BWANA,[#Law 8:35; 1 Nya 9:33; Zab 130:6; Lk 2:37]

Mhimidini BWANA, nyote pia.

Ninyi mnaosimama usiku

Katika nyumba ya BWANA.

2Painulieni patakatifu mikono yenu,[#Zab 28:2; 1 Tim 2:8]

Na kumhimidi BWANA.

3BWANA akubariki toka Sayuni,[#Zab 124:8; 128:5]

Aliyezifanya mbingu na nchi.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania