The chat will start when you send the first message.
1Ee BWANA, nimekuita, unijie hima,
Uisikie sauti yangu nikuitapo.
2Sala yangu ipae mbele zako kama uvumba,[#Efe 5:2; 1 Tim 2:8; Ufu 5:8]
Kuinuliwa mikono yangu kama dhabihu ya jioni.
3Ee BWANA, uweke mlinzi kinywani pangu,
Mngojezi mlangoni pa midomo yangu.
4Usiuelekeze moyo wangu kunako jambo baya,[#Mt 6:14; 20:15; Mit 23:6]
Nisiyazoelee matendo yasiyofaa,
Pamoja na watu watendao maovu;
Wala nisile vyakula vyao vya anasa.
5Mwenye haki na anipige, itakuwa fadhili;
Anikemee, itakuwa kama mafuta kichwani;
Kichwa changu kisikatae,
Maana siachi kusali kati ya mabaya yao.
6Makadhi wao wakiangushwa kando ya genge,
Watayasikia maneno yangu, maana ni matamu.
7Kama kupasua kuni na kuzichanja juu ya nchi,[#2 Kor 1:9]
Ndivyo ilivyo mifupa yetu mdomoni pa kuzimu.
8Macho yangu yanakuelekea Wewe, MUNGU Bwana,[#Zab 25:15]
Nimekukimbilia Wewe, usiniache nafsi yangu.
9Unilinde na mtego walionitegea,
Na matanzi yao watendao maovu.
10Wabaya na waanguke katika nyavu zao wenyewe,[#Est 7:10; Zab 7:15]
Pindi mimi ninapopita salama.