Zab 146

Zab 146

Sifa kwa Kupata Msaada wa Mungu

1Haleluya.[#146:1 maana yake ni, Msifuni BWANA.]

Ee nafsi yangu, umsifu BWANA.

2Nitamsifu BWANA muda ninaoishi,

Nitamwimbia Mungu wangu ningali ni hai.

3Msiwatumainie wakuu,[#Isa 2:22]

Wala binadamu ambaye hakuna wokovu kwake.

4Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake,[#Mhu 12:7; 1 Kor 2:6]

Siku hiyo mawazo yake yapotea.

5Heri ambaye Mungu wa Yakobo ni msaada wake,[#Yer 17:7]

Na tumaini lake ni kwa BWANA, Mungu wake,

6Aliyezifanya mbingu na nchi,[#Mik 7:20; Mdo 4:24; 14:15; Ufu 14:7]

Bahari na vitu vyote vilivyomo.

Huishika kweli milele,

7Huwafanyia hukumu walioonewa,

Huwapa wenye njaa chakula;

BWANA hufungua waliofungwa;

8BWANA huwafumbua macho waliopofuka;

BWANA huwainua walioinama;

BWANA huwapenda wenye haki;

9BWANA huwahifadhi wageni;

Huwategemeza yatima na mjane;

Bali njia ya wasio haki huipotosha.

10BWANA atamiliki milele,

Mungu wako, Ee Sayuni, kizazi hata kizazi.

Haleluya.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania