Zab 16

Zab 16

Wimbo wa Imani na Usalama kwa Mungu

1Mungu, unihifadhi mimi,[#Zab 25:20]

Kwa maana nakukimbilia Wewe.

2Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;

Sina wema ila utokao kwako.

3Watakatifu waliopo duniani ndio Walio bora,

Hao ndio niliopendezwa nao.

4Huzuni zao zitaongezeka

Wambadilio Mungu kwa mwingine;

Sitazimimina sadaka zao za damu,

Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.

5BWANA ndiye fungu la posho langu,

Na la kikombe changu;

Wewe unaishika kura yangu.

6Kamba zangu zimeniangukia mahali pema,

Naam, nimepata urithi mzuri.

7Nitamhimidi BWANA aliyenipa shauri,

Naam, mtima wangu umenifundisha usiku.

8Nimemweka BWANA mbele yangu daima,[#Mdo 2:25-28]

Kwa kuwa yuko kuumeni kwangu, sitaondoshwa.

9Kwa hiyo moyo wangu unafurahi,

Nao utukufu wangu unashangilia,

Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.

10Maana hutakuachia kuzimu nafsi yangu,[#Mdo 13:35; Zab 49:15; Mdo 2:27; Dan 9:24; Lk 1:35]

Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.

11Utanijulisha njia ya uzima;[#Mdo 2:28]

Mbele za uso wako ziko furaha tele;

Na katika mkono wako wa kuume

Mna mema ya milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania