Zab 30

Zab 30

Shukrani kwa Kuponywa Maradhi Mabaya

1Ee BWANA, nitakutukuza kwa maana umeniinua,

Wala hukuwafurahisha adui zangu juu yangu.

2Ee BWANA, Mungu wangu,[#Zab 6:2-4]

Nalikulilia ukaniponya.

3Umeniinua nafsi yangu,[#Zab 40:1,2]

Ee BWANA, kutoka kuzimu.

Umenihuisha na kunitoa

Miongoni mwao washukao shimoni.

4Mwimbieni BWANA zaburi,

Enyi watauwa wake.

Na kufanya shukrani.

Kwa kumbukumbu la utakatifu wake.

5Maana ghadhabu zake ni za kitambo kidogo,[#Zab 16:11; Ufu 22:17]

Katika radhi yake mna uhai.

Huenda kilio huja kukaa usiku,

Lakini asubuhi huwa furaha.

6Nami nilipofanikiwa nalisema,[#Ayu 29:18]

Sitaondoshwa milele.

7BWANA, kwa radhi yako[#Zab 104:29]

Wewe uliuimarisha mlima wangu.

Uliuficha uso wako,

Nami nikafadhaika.

8Ee BWANA, nalikulilia Wewe,

Naam, kwa BWANA naliomba dua.

9Mna faida gani katika damu yangu[#Zab 115:17]

Nishukapo shimoni?

Mavumbi yatakusifu?

Yataitangaza kweli yako?

10Ee BWANA, usikie, unirehemu,[#Zab 4:1]

BWANA, uwe msaidizi wangu.

11Uligeuza matanga yangu kuwa machezo;[#2 Sam 6:14]

Ulinivua gunia, ukanivika furaha.

12Ili utukufu wangu ukusifu,

Wala usinyamaze.

Ee BWANA, Mungu wangu,

Nitakushukuru milele.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania