Zab 36

Zab 36

Uovu wa Watu na Wema wa Mungu

1Kuasi kwake yule mwovu hunena moyoni mwake,[#Rum 3:18; Mwa 20:11; Mit 8:13; Mhu 12:3]

Hakuna hofu ya Mungu mbele ya macho yake.

2Kwa maana hujipendekeza machoni pake

Kuwa upotovu wake hautaonekana na kuchukiwa.

3Maneno ya kinywa chake ni uovu na hila,[#Yer 4:22]

Ameacha kuwa na akili na kutenda mema.

4Huwaza maovu kitandani pake,[#Mik 2:1; Isa 65:2]

Hujiweka katika njia mbaya; ubaya hauchukii.

5Ee BWANA, fadhili zako zafika hata mbinguni,[#Zab 57:10]

Uaminifu wako hata mawinguni.

6Haki yako ni kama milima ya Mungu,[#Ayu 11:8; Rum 11:33; Ayu 7:20; Zab 145:9]

Hukumu zako ni vilindi vikuu,

Ee BWANA, unawaokoa wanadamu na wanyama.

7Ee Mungu, jinsi zilivyo na thamani fadhili zako![#Rut 2:12]

Wanadamu huukimbilia uvuli wa mbawa zako.

8Watashibishwa kwa unono wa nyumba yako,[#Ayu 20:17; Ufu 22:1]

Nawe utawanywesha mto wa furaha zako.

9Maana kwako Wewe iko chemchemi ya uzima,[#Isa 12:3; Yer 2:13; Zek 13:1; Yn 4:10,14; Ufu 21:6; Mdo 26:18; Efe 5:8; Kol 1:13; 1 Pet 2:9]

Katika nuru yako tutaona nuru.

10Uwadumishie wakujuao fadhili zako,[#Yer 22:16]

Na wanyofu wa moyo uaminifu wako.

11Mguu wa kiburi usinikaribie,

Wala mkono wa wasio haki usinifukuze.

12Huko ndiko walikoanguka wafanyao maovu;

Wameangushwa chini wasiweze kusimama.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania