Zab 43

Zab 43

Sala kwa Mungu Wakati wa Shida

1Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki,[#Zab 7:8]

Uniokoe na mtu wa hila asiye haki.

2Kwa kuwa Wewe ndiwe Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa?[#Zab 28:7; Isa 26:4]

Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?

3Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze,[#Zab 2:6; 3:4]

Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.

4Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye

furaha yangu na shangwe yangu;

Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.

5Nafsi yangu, kwa nini kuinama,[#Zab 42:5,11]

Na kufadhaika ndani yangu?

Umtumaini Mungu;

Kwa maana nitakuja kumsifu,

Aliye afya ya uso wangu,

Na Mungu wangu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania