The chat will start when you send the first message.
1Moyo wangu umefurika kwa neno jema,
Mimi nasema niliyomfanyizia mfalme;
Ulimi wangu ni kalamu ya mwandishi mstadi.
2Wewe u mzuri sana kuliko wanadamu;
Neema imemiminiwa midomoni mwako,
Kwa hiyo Mungu amekubariki hata milele.
3Jifungie upanga wako pajani, wewe uliye hodari,
Utukufu ni wako na fahari ni yako.
4Katika fahari yako usitawi uendelee
Kwa ajili ya kweli na upole na haki
Na mkono wako wa kuume
Utakufundisha mambo ya kutisha.
5Mishale yako ni mikali, watu huanguka chini yako;
Imo mioyoni mwa adui za mfalme.
6Kiti chako cha enzi, Mungu, ni cha milele na milele,[#Ebr 1:8-9; Zab 93:2; Isa 9:6,7]
Fimbo ya ufalme wako ni fimbo ya adili.
7Umeipenda haki;[#Zab 33:5; Mt 3:15; Ebr 1:9; Isa 61:1; Yn 20:17]
Umeichukia dhuluma.
Kwa hiyo MUNGU, Mungu wako, amekupaka mafuta,
Mafuta ya furaha kuliko wenzako.
8Mavazi yako yote hunukia manemane
Na udi na mdalasini.
Katika majumba ya pembe
Vinubi vimekufurahisha.
9Binti za wafalme wamo
Miongoni mwa akina bibi wako wastahiki.
Mkono wako wa kuume amesimama malkia
Amevaa dhahabu ya Ofiri.
10Sikia, binti, utazame, utege sikio lako,[#Kum 21:13]
Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako.
11Naye mfalme atautamani uzuri wako,[#Zab 95:6; Isa 54:5]
Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie.
12Na binti Tiro analeta kipawa chake,
Nao matajiri wa watu watajipendekeza kwako.
13Binti mfalme yumo ndani ana fahari tupu,[#Ufu 19:7,8]
Mavazi yake ni ya nyuzi za dhahabu.
14Atapelekwa kwa mfalme
Na mavazi yaliyofumwa kwa uzuri.
Wanawali wenzake wanaomfuata,
Watapelekwa kwako.
15Watapelekwa kwa furaha na shangwe,
Na kuingia katika nyumba ya mfalme.
16Badala ya baba zako watakuwapo watoto wako,[#1 Pet 2:9; Ufu 1:6]
Utawafanya kuwa wakuu katika nchi zote.
17Jina lako nitalifanya kuwa kumbukumbu[#Isa 11:10; Mal 1:11]
Katika vizazi vyote.
Kwa hiyo mataifa watakushukuru
Milele na milele.