Zab 46

Zab 46

Ulinzi wa Mungu kwa Mji na Watu Wake

1Mungu kwetu sisi ni kimbilio na nguvu,

Msaada utakaoonekana tele wakati wa mateso.

2Kwa hiyo hatutaogopa ijapobadilika nchi,

Ijapotetemeka milima moyoni mwa bahari.

3Maji yake yajapovuma na kuumuka,

Ijapopepesuka milima kwa kiburi chake.

4Kuna mto, vijito vyake vyaufurahisha mji wa Mungu,[#Isa 8:7; Ufu 22:1; 2 Nya 6:6; Zab 48:1; Isa 60:14; Ebr 12:22]

Patakatifu pa maskani zake Aliye juu.

5Mungu yu katikati yake hautatetemeshwa;[#Kum 23:14; Isa 12:6; Eze 43:7]

Mungu atausaidia asubuhi na mapema.

6Mataifa yalighadhibika, falme zikataharuki;

Alitoa sauti yake, nchi ikayeyuka.

7BWANA wa majeshi yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

8Njoni myatazame matendo ya BWANA,

Jinsi alivyofanya ukiwa katika nchi.

9Avikomesha vita hata mwisho wa dunia;

Avunja uta, akata mkuki, achoma moto magari.

10Acheni, mjue ya kuwa Mimi ni Mungu,

Nitakuzwa katika mataifa, nitakuzwa katika nchi.

11BWANA wa majeshi yu pamoja nasi,

Mungu wa Yakobo ni ngome yetu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania