Zab 57

Zab 57

Sifa na Hakikisho katika Mateso

1Unirehemu, Ee Mungu, unirehemu mimi,[#Isa 26:20]

Maana nafsi yangu imekukimbilia Wewe.

Nitaukimbilia uvuli wa mbawa zako,

Hata misiba hii itakapopita.

2Nitamwita MUNGU Aliye juu,[#Zab 138:8]

Mungu anitimiziaye mambo yangu.

3Atapeleka toka mbinguni na kuniokoa,[#Zab 144:5; 40:11]

Atukanapo yule atakaye kunimeza.

Mungu atazipeleka

Fadhili zake na kweli yake

4Nafsi yangu i kati ya simba,[#Mit 30:14; Zab 64:3]

Nitastarehe kati yao waliowaka moto.

Wanadamu meno yao ni mikuki na mishale,

Na ndimi zao ni upanga mkali.

5Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,[#Zab 108:5]

Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

6Wameweka wavu ili kuninasa miguu;[#Zab 9:15]

Nafsi yangu imeinama;

Wamechimba shimo mbele yangu;

Wametumbukia ndani yake!

7Ee Mungu, moyo wangu u thabiti,[#Zab 108:1]

Moyo wangu u thabiti.

Nitaimba, nitaimba zaburi,

8Amka, utukufu wangu.[#Amu 5:12]

Amka, kinanda na kinubi,

Nitaamka alfajiri.

9Ee Bwana, nitakushukuru kati ya watu,

Nitakuimbia zaburi kati ya mataifa.

10Maana fadhili zako ni kubwa hata mbinguni,[#Zab 108:4]

Na uaminifu wako hata mawinguni.

11Ee Mungu, utukuzwe juu ya mbingu,

Na juu ya nchi yote uwe utukufu wako.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania