Zab 61

Zab 61

Hakikisho la Ulinzi wa Mungu

1Ee Mungu, ukisikie kilio changu,

Uyasikilize maombi yangu.

2Toka mwisho wa nchi nitakulilia nikizimia moyo,[#1 Tim 2:8]

Uniongoze juu ya mwamba nisioweza kuupanda.

3Kwa maana ulikuwa kimbilio langu,[#Mit 18:10]

Ngome yenye nguvu adui asinipate.

4Nitakaa katika hema yako milele,[#Zab 15:1; 23:6; Ufu 3:12]

Nitaikimbilia sitara ya mbawa zako

5Maana Wewe, Mungu, umezisikia nadhiri zangu.[#1 Kor 3:21-23]

Umewapa urithi wao waliogopao jina lako.

6Utaziongeza siku za mfalme,

Miaka yake itakuwa kama vizazi vingi.

7Atakaa mbele za Mungu milele,[#Zab 41:12; Lk 1:32]

Ziagize fadhili na kweli zimhifadhi.

8Ndivyo nitakavyoliimbia jina lako daima,[#Zab 56:12]

Ili niondoe nadhiri zangu kila siku.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania