Zab 64

Zab 64

Sala ya Ulinzi kutoka kwa Adui

1Mungu, uisikie sauti yangu katika malalamiko yangu;

Unilinde uhai wangu na hofu ya adui.

2Utanificha mbali na shauri la siri la watenda mabaya,[#Zab 143:9]

Mbali na ghasia ya watu wafanyao maovu;

3Waliounoa ulimi wao kama upanga,[#Zab 57:4]

Wameielekeza mishale yao, maneno ya uchungu,

4Wapate kumpiga mkamilifu faraghani,

Kwa ghafula humpiga wala hawaogopi.

5Walijifanya hodari katika jambo baya;

Hushauriana juu ya kutega mitego;

Husema, Ni nani atakayeiona?

6Hutunga maovu; husema, Tumefanya shauri kamili;

Na mawazo ya ndani ya kila mmoja wao,

Na moyo wake, huwa siri kabisa.

7Kwa hiyo Mungu atawapiga shabaha,

Kwa mshale mara watapigwa.

8Ndivyo watakavyokwazwa,[#Mit 12:13]

Ulimi wao wenyewe ukishindana nao.

Wote wawaonao watatikisa kichwa.

9Na watu wote wataogopa,

Wataitangaza kazi ya Mungu,

Na kuyafahamu matendo yake.

10Mwenye haki atamfurahia BWANA na kumkimbilia,[#Zab 32:11; Flp 4:4]

Na wote wenye moyo wa adili watajisifu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania