The chat will start when you send the first message.
1Nimpazie Mungu sauti yangu,
Naam, nimpazie Mungu, naye atanisikia.
2Siku ya taabu yangu nalimtafuta Bwana;[#Zab 50:15; Isa 26:9]
Mkono wangu ulinyoshwa usiku, haukulegea;
Nafsi yangu ilikataa kufarijika.
3Nilipotaka kumkumbuka Mungu nalifadhaika;
Nilipotaka kutafakari roho yangu ilizimia.
4Ulizishika kope za macho yangu zisifumbike;
Naliona mashaka nisiweze kunena.
5Nalifikiri habari za siku za kale,[#Kum 32:7; Zab 14:5; Isa 51:9]
Miaka ya zamani zilizopita.
6Nakumbuka wimbo wangu usiku,
Nawaza moyoni mwangu,
Roho yangu ikatafuta.
7Je! Bwana atatupa milele na milele?
Hatatenda fadhili tena kabisa?
8Rehema zake zimekoma hata milele?[#Isa 27:11; Yon 2:4; Hes 23:19; Yer 15:18; Rum 9:6]
Ahadi yake imekwisha hata vizazi vyote?
9Mungu amesahau fadhili zake?[#Isa 49:15]
Amezuia kwa hasira rehema zake?
10Nikasema, Ndio udhaifu wangu huo;[#Ayu 42:3; Zab 31:22; Yer 10:19]
Lakini nitaikumbuka miaka ya mkono wa kuume wake Aliye juu.
11Nitayakumbuka matendo ya BWANA;[#1 Nya 16:12; Zab 28:5; Isa 5:1]
Naam, nitayakumbuka maajabu yako ya kale.
12Pia nitaitafakari kazi yako yote;
Nitaziwaza habari za matendo yako.
13Ee Mungu, njia yako i katika utakatifu;[#Zab 73:17]
Ni nani aliye mungu mkuu kama Mungu?
14Wewe ndiwe Mungu ufanyaye maajabu;
Uliudhihirisha uweza wako kati ya mataifa.
15Kwa mkono wako umewakomboa watu wako,
Wana wa Yakobo na Yusufu.
16Ee Mungu, yale maji yalikuona,[#Kut 14:21; Yos 3:15,16]
Yale maji yalikuona, yakaogopa.
Vilindi vya maji navyo vikatetemeka,
17Mawingu yakamwaga maji.
Mbingu nazo zikatoa sauti,
Mishale yako nayo ikatapakaa.
18Sauti ya radi yako ikawa katika kisulisuli;
Umeme uliuangaza ulimwengu.
Nchi ilitetemeka na kutikisika;
19Njia yako ilikuwa katika bahari.[#Hab 3:15; Kut 14:28; Ayu 37:23]
Na mapito yako yalikuwa katika maji makuu;
Hatua zako hazikujulikana.
20Uliwaongoza watu wako kama kundi,[#Isa 63:11]
Kwa mkono wa Musa na Haruni.