The chat will start when you send the first message.
1Wewe, MUNGU, Bwana wetu
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!
Wewe umeuweka utukufu wako mbinguni;
2Vinywani mwa watoto wachanga na wanyonyao[#Mt 21:16; 11:25; 1 Kor 1:27]
Umeiweka misingi ya nguvu;
Kwa sababu yao wanaoshindana nawe;
Uwakomeshe adui na mijilipiza kisasi.
3Nikiziangalia mbingu zako, kazi ya vidole vyako,[#Zab 44:16; 19:1; Ayu 22:12; Rum 1:20]
Mwezi na nyota ulizoziratibisha;
4Mtu ni kitu gani hata umkumbuke,[#Ayu 7:17-18; Zab 144:3; Ebr 2:6-8]
Na binadamu hata umwangalie?
5Umemfanya mdogo punde kuliko Mungu;
Umemvika taji ya utukufu na heshima;
6Umemtawaza juu ya kazi za mikono yako;[#1 Kor 15:27; Efe 1:22; Ebr 2:8; Mwa 1:26]
Umevitia vitu vyote chini ya miguu yake.
7Kondoo, na ng’ombe wote pia;
Naam, na wanyama wa kondeni;
8Ndege wa angani, na samaki wa baharini;
Na kila kipitacho njia za baharini.
9Wewe, MUNGU, Bwana wetu,[#Ayu 11:7; Zab 35:10]
Jinsi lilivyo tukufu jina lako duniani mwote!