Zab 87

Zab 87

Shangwe ya Kuishi Sayuni

1Msingi wake upo

Juu ya milima mitakatifu.

2BWANA ayapenda malango ya Sayuni

Kuliko maskani zote za Yakobo.

3Umetajwa kwa mambo matukufu,[#Isa 60:1]

Ee Mji wa Mungu.

4Nitataja Rahabu na Babeli

Miongoni mwao wanaonijua.

Tazama Filisti, na Tiro, na Kushi;

Huyu alizaliwa humo.

5Naam, mintarafu Sayuni itasemwa,[#Eze 48:35; Mt 16:18]

Huyu na huyu alizaliwa humo.

Na Yeye Aliye juu

Ataufanya imara.

6BWANA atahesabu, awaandikapo mataifa,[#Zab 22:30; Isa 4:3; Yer 3:19; Eze 13:9]

Huyu alizaliwa humo.

7Waimbao na wachezao na waseme,

Visima vyangu vyote vimo mwako.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania