Zab 91

Zab 91

Hakikisho la Ulinzi wa Mungu

1Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu

Atakaa katika uvuli wake Mwenyezi.

2Nitasema, BWANA ndiye kimbilio langu na ngome yangu,

Mungu wangu nitakayemtumaini.

3Maana Yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji,

Na katika tauni iharibuyo.

4Kwa manyoya yake atakufunika,[#Zab 61:4]

Chini ya mbawa zake utapata kimbilio;

Uaminifu wake ni ngao na kigao.

5Hutaogopa hofu ya usiku,[#Ayu 5:19; Mit 3:23; Isa 43:2]

Wala mshale urukao mchana,

6Wala tauni ipitayo gizani,

Wala uele uharibuo adhuhuri,

7Ijapo watu elfu waanguka ubavuni pako.

Naam, kumi elfu mkono wako wa kuume!

Hata hivyo hautakukaribia wewe.

8Ila kwa macho yako utatazama,[#Mal 1:5]

Na kuyaona malipo ya wasio haki.

9Kwa kuwa Wewe BWANA ndiwe kimbilio langu;

Umemfanya Aliye juu kuwa makao yako.

10Mabaya hayatakupata wewe,[#Mit 1:33; 2 The 3:3; 2 Pet 2:9]

Wala tauni haitaikaribia hema yako.

11Kwa kuwa atakuagizia malaika zake[#Mt 4:6; Lk 4:10; #Zab 34:7; Mt 4:6; Lk 4:10; Ebr 1:14]

Wakulinde katika njia zako zote.

12Mikononi mwao watakuchukua,[#Ayu 5:23; Zab 37:24; Mt 4:6; Lk 4:11]

Usije ukajikwaa mguu wako katika jiwe.

13Utawakanyaga simba na nyoka,[#Lk 10:19]

Mwana-simba na joka utawaseta kwa miguu.

14Kwa kuwa amekaza kunipenda

Nitamwokoa; na kumweka palipo juu,

Kwa kuwa amenijua Jina langu.

15Ataniita nami nitamwitikia;[#Ayu 22:27; Zab 18:3; Yer 33:3; Zek 13:9; Ebr 5:7; Zab 43:2; 1 Sam 2:30]

Nitakuwa pamoja naye taabuni,

Nitamwokoa na kumtukuza;

16Kwa siku nyingi nitamshibisha,

Nami nitamwonyesha wokovu wangu.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania