Zab 98

Zab 98

Sifa kwa Mwamuzi wa Dunia

1Mwimbieni BWANA wimbo mpya,[#Isa 59:16]

Kwa maana ametenda mambo ya ajabu.

Mkono wa kuume wake mwenyewe,

Mkono wake mtakatifu umemtendea wokovu.

2BWANA ameufunua wokovu wake,[#Isa 52:10; Lk 2:30; Isa 62:2; Rum 3:25; Kum 4:31; Mik 7:20; Lk 1:54; Isa 49:6; Lk 3:6; Mdo 13:47]

Machoni pa mataifa ameidhihirisha haki yake.

3Amezikumbuka rehema zake,

Na uaminifu wake kwa nyumba ya Israeli.

Miisho yote ya dunia imeuona

Wokovu wa Mungu wetu.

4Mshangilieni BWANA, nchi yote,

Inueni sauti, imbeni kwa furaha, imbeni zaburi.

5Mwimbieni BWANA zaburi kwa kinubi,

Kwa kinubi na sauti ya zaburi.

6Kwa panda na sauti ya baragumu.[#Hes 10:10; 1 Nya 15:28; 2 Nya 29:27]

Shangilieni mbele za Mfalme, BWANA.

7Bahari na ivume na vyote viijazavyo,

Ulimwengu nao wanaokaa ndani yake.

8Mito na ipige makofi,

Milima na iimbe pamoja kwa furaha.

9Mbele za BWANA;

Kwa maana anakuja aihukumu nchi.

Atauhukumu ulimwengu kwa haki,

Na mataifa kwa adili.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania