Wim 3

Wim 3

Ndoto za Mapenzi

1Usiku kitandani nalimtafuta mpendwa wa nafsi yangu,[#Zab 4:6; 6:6; Isa 26:9]

Nalimtafuta, nisimpate.

2Nikasema, Haya, niondoke nizunguke mjini,

Katika njia zake na viwanjani,

Nimtafute mpendwa wa nafsi yangu.

Nikamtafuta, nisimpate.

3Walinzi wazungukao mjini waliniona;[#Wim 5:7; Isa 21:6-8,11,12]

Je! Mmemwona mpendwa wa nafsi yangu?

4Kitambo kidogo tu nikiisha kuwaondokea,[#Mit 8:17; 4:13; Rum 8:35,39]

Nikamwona mpendwa wa nafsi yangu;

Nikamshika, nisimwache tena,

Hata nilipomleta nyumbani mwa mamangu,

Chumbani mwake aliyenizaa.

5Nawasihi, enyi binti za Yerusalemu,[#Wim 2:7]

Kwa paa na kwa ayala wa porini,

Msiyachochee mapenzi, wala kuyaamsha,

Hata yatakapoona vema yenyewe.

Bwana Arusi na Kundi lake Wakaribia

6Ni nani huyu apandaye kutoka nyikani,[#Wim 8:5; Yer 2:2]

Mfano wake ni nguzo za moshi;

Afukizwa manemane na ubani,

Na mavumbi ya manukato yote ya mchuuzi?

7Tazama, ni machela yake Sulemani;

Mashujaa sitini waizunguka,

Wa mashujaa wa Israeli.

8Wote wameshika upanga,

Wamehitimu kupigana;

Kila mtu anao upanga wake pajani

Kwa hofu ya kamsa za usiku.

9Mfalme Sulemani alijifanyizia machela

Ya miti ya Lebanoni;

10Nguzo zake alizifanyiza za fedha,[#Mt 22:37; Yn 13:1,34; Rum 5:8; Efe 3:19; 1 Pet 1:7,8]

Na mgongo wake wa dhahabu,

Kiti chake kimepambwa urujuani,

Gari lake limenakishiwa njumu,

Hiba ya binti za Yerusalemu.

11Tokeni, enyi binti za Sayuni,[#Ufu 11:15; Zab 110:3; Isa 62:5]

Mtazameni Mfalme Sulemani,

Amevaa taji alivyovikwa na mamaye,

Siku ya maposo yake,

Siku ya furaha ya moyo wake.

Swahili Union Version (SUV): © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 1952, 1997. All rights reserved. lt/pgt ltpgtSwahili Union Version (SUV): Hakimiliki -1952, 1997: kwa: Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya. Haki zote zimehifadhiwa.
Published by: Bible Society of Tanzania