Ufunuo 1

Ufunuo 1

Yohana Aeleza Kuhusu Kitabu Hiki

1Huu ni ufunuo kutoka kwa Yesu Kristo, ambao Mungu alimpa ili awaoneshe watumishi wake yale ambayo ni lazima yatokee muda mfupi ujao. Yesu Kristo alimtuma malaika wake ili amwonyeshe Yohana, mtumishi wake,[#1:1 Utangulizi (kujulisha) wa ukweli uliofichwa.]

2ambaye amesema kila kitu alichokiona. Ni ukweli alioambiwa na Yesu Kristo; ni ujumbe kutoka kwa Mungu.

3Ana heri anayesoma maneno ya ujumbe huu kutoka kwa Mungu kwa kupaza sauti na wale wanaousikia ujumbe huu na kuyatendea kazi yaliyoandikwa ndani yake. Wakati uliosalia ni mfupi.

Yohana Ayaandikia Makanisa

4Kutoka kwa Yohana,

Kwenda kwa makanisa saba yaliyo katika Asia:

Agano Jipya: Tafsiri ya Kusoma-Kwa-Urahisi Toleo la Awali © 2017 Bible League International
Published by: Bible League International