Amosi 4

Mapatilizo yao wanawake wa Waisiraeli wote.

1Lisikieni neno hili, ninyi ng'ombe wa Basani!

Ninyi mlioko milimani kwa Samaria

mkiwakorofisha wanyonge na kuwaponda maskini!

Ninyi mnaowaambia bwana zao: Haya! Leteni, tunywe!

2Bwana Mungu ameapa na kuutaja utukufu wake kwamba:

Mtaona, siku zikiwajia ninyi,

mtakapovutwa juu kwa kulabu,

hata masazo yenu yatavutwa juu kwa ndoana za kuvulia

samaki.

3Mtatoka penye nyufa za ukuta,

kila mwanamke mmoja ashike njia yake ya kwenda moja kwa

moja,

mje kujitupa huko Harmoni; ndivyo, asemavyo Bwana.

4Haya! Nendeni Beteli, mjikoseshe!

Nendeni Gilgali, mzidishe kujikosesha!

Katoeni asubuhi vipaji vyenu vya tambiko!

Hata kila siku ya tatu yatoeni mafungu yenu ya kumi!

5Chomeni mikate yenye chachu, iwe shukrani!

Tangazeni, visikilike, watu watoe vipaji viwapendezavyo!

Kwani ndivyo, mnavyovipenda, ninyi wana wa Isiraeli;

ndivyo, asemavyo Bwana Mungu.

6Nami niliwapa meno yakosayo kazi mijini mwenu mote

nao ukosefu wa mkate pote, mnapokaa, lakini hamkurudi

kwangu;

ndivyo, asemavyo Bwana.

7Tena mimi niliwanyima mvua,

miezi mitatu tu ilipokuwa imesalia mpaka mavunoni,

mji mmoja nikaunyeshea mvua, tena mwingine sikuunyeshea

mvua,

shamba moja likanyeshewa na mvua, jingine lisilopata mvua likakauka.

8Miji miwili mitatu ikatangatanga kuendea mji mmoja tu,

ndimo wapate kunywa maji, ijapo wasishibe, lakini

hamkurudi kwangu;

ndivyo, asemavyo Bwana.

9Nikawapiga ninyi, nikayaunguza mashamba na kuyakausha

kabisa,

tena mara nyingi nzige waliyala kwenu

mashamba na mizabibu na mikuyu na michekele yenu,

lakini hamkurudi kwangu;

ndivyo, asemavyo Bwana.

10Nilituma kwenu magonjwa mabaya, kama nilivyovifanya huko

Misri,

nikawaua vijana wenu kwa panga, nao farasi wenu

wakatekwa.

Nikaupandisha mnuko mbaya wa kambi zenu, uingie puani

mwenu,

lakini hamkurudi kwangu;

ndivyo, asemavyo Bwana.

11Niliwafudikiza wa kwenu, kama Mungu alivyofudikiza Sodomu

na Gomora,

mkawa kama kijinga kilichopona kwa kuokolewa,

kisiteketee chote motoni, lakini hamkurudi kwangu;

ndivyo, asemavyo Bwana.

12Kwa hiyo yako, nitakayokufanyizia Isiraeli;

jiweke tayari kukutana na Mungu wako, Isiraeli,

kwa ajili yao nitakayokufanyzia!

13Kwani utamwona atengenezaye milima, aumbaye upepo,

amwambiaye mtu ayawazayo moyoni mwake,

ni yeye ayageuzaye mapema kuwa giza

akipita na kukanyaga juu ya vilima vya nchi;

Bwana Mungu Mwenye vikosi ni Jina lake.

Swahili Roehl Bible 1937 © Bible Society of Tanzania, 1937.
Published by: Bible Society of Tanzania