The chat will start when you send the first message.
1Haya, shuka, keti mavumbini,[#Yer 48:18; Omb 2:3,10; Isa 13:1—14:23; Yer 50:1—51:64]
Ewe bikira, binti Babeli;
Keti chini pasipo kiti cha enzi,
Ewe binti wa Wakaldayo;
Maana hutaitwa tena mwororo, mpenda anasa.
2Twaa mawe ya kusagia, usage unga;[#Kut 11:5]
Vua utaji wako, ondoa mavazi yako,
Funua mguu wako, pita katika mito ya maji.
3Uchi wako utafunuliwa,[#Nah 3:5; Mt 7:2; Rum 12:19]
Naam, aibu yako itaonekana.
Nitalipa kisasi; simkubali mtu ye yote.
4Mkombozi wetu, BWANA wa majeshi ndilo jina lake,
Mtakatifu wa Israeli.
5Kaa kimya, ingia gizani,[#1 Sam 2:9; Dan 2:37]
Ee binti wa Wakaldayo;
Maana hutaitwa tena Malkia wa falme.
6Nalikuwa nimekasirika na watu wangu, naliutia unajisi urithi wangu, nikawatia mkononi mwako; wewe hukuwatendea rehema; uliwatia wazee nira yako, nayo nzito sana.[#2 Nya 28:9; Isa 10:6; Zek 1:15; Kum 28:50]
7Ukasema, Mimi nitakuwa bibi milele; hata hukuyatia hayo moyoni mwako, wala hukukumbuka mwisho wa mambo hayo.[#Ufu 18:7]
8Sasa, basi, sikia haya, wewe upendaye anasa, ukaaye na kujiona salama, wewe usemaye moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi; sitaketi mfano wa mjane, wala sitajua kufiwa na watoto;[#Sef 2:15; Ufu 18:7-8]
9lakini mambo haya mawili yatakupata katika dakika moja siku moja, kufiwa na watoto, na ujane; yatakupata kiasi kitimilifu, uchawi wako ujapokuwa mwingi, na uganga wako mwingi mno.[#1 The 5:3; Dan 2:2; Nah 3:4; 2 The 2:9,10; Ufu 9:21]
10Maana umeutumainia ubaya wako; umesema, Hapana anionaye; hekima yako, na maarifa yako yamekupotosha, nawe umesema moyoni mwako, Mimi ndiye, wala hapana mwingine zaidi yangu mimi.[#Zab 52:7; Eze 8:12]
11Kwa sababu hiyo ubaya utakupata; wala hutajua kutopoa kwake; na msiba utakuangukia; hutaweza kuuondoa; na ukiwa utakupata kwa ghafula, usioujua.[#Isa 13:6; Dan 5:30; Lk 17:27]
12Simama sasa na uganga wako, na wingi wa uchawi wako, uliojitaabisha nao tangu ujana wako; labda utaweza kupata faida, labda utaweza kushinda.
13Umechoka kwa wingi wa mashauri yako; basi, na wasimame hao wajuao falaki, wazitazamao nyota, watabirio kila mwezi mambo ya mwezi huo, wakakuokoe na mambo yatakayokupata.
14Tazama, watakuwa kama mabua makavu; moto utawateketeza; hawatajiokoa na nguvu za mwali wa moto; hautakuwa kaa la kukota moto, wala moto wa kukaa karibu nao.[#Nah 1:10; Mal 4:1]
15Ndivyo yatakavyokuwa mambo hayo uliyojitaabisha nayo; wale waliofanya biashara nawe tangu ujana wako watatanga-tanga mbali nawe, kila mtu akienda zake; hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.[#Ufu 18:11]