Zaburi 124

Zaburi 124

Mungu kinga yetu

1“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu…”

Semeni nyote mlio katika Israeli:

2“Kama Mwenyezi-Mungu asingalikuwa upande wetu,

wakati ule tuliposhambuliwa na maadui,

3hakika tungalimezwa tukiwa hai,

wakati hasira zao zilipotuwakia.

4Tungalikumbwa na gharika,

tungalifunikwa na mto wa maji,

5mkondo wa maji ungalituchukua!”

6Atukuzwe Mwenyezi-Mungu,

ambaye hakutuacha makuchani mwao.

7Tumeponyoka kama ndege mtegoni;

mtego umeteguliwa, nasi tukaokoka.

8Msaada wetu watoka kwa Mwenyezi-Mungu,

aliyeumba mbingu na dunia.

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania