The chat will start when you send the first message.
1Kando ya mito ya Babuloni, tulikaa,[#137:1 Yaani mifereji na vijito vya mito ya Tigri na Eufrate.]
tukawa tunalia tulipokumbuka Siyoni.
2Katika miti ya nchi ile,
tulitundika zeze zetu.
3Waliotuteka walitutaka tuwaimbie;
watesi wetu walitutaka tuwafurahishe:
“Tuimbieni mojawapo ya nyimbo za Siyoni!”
4Twawezaje kuimba wimbo wa Mwenyezi-Mungu
katika nchi ya kigeni?
5Ee Yerusalemu, kama nikikusahau,
mkono wangu wa kulia na ukauke!
6Ulimi wangu na uwe mzito,
kama nisipokukumbuka wewe, ee Yerusalemu;
naam, nisipokuthamini kuliko furaha yangu kubwa!
7Ee Mwenyezi-Mungu, usisahau waliyotenda Waedomu,[#137:7 Huenda Waedomu walifurahi wakati mji wa Yerusalemu ulipoteketezwa na Wababuloni na wengi wa wakazi wake wakachukuliwa mateka. Taz Eze 35:5-15; Oba 10-14.]
siku ile Yerusalemu ilipotekwa;
kumbuka waliyosema:
“Bomoeni mji wa Yerusalemu!
Ng'oeni hata na misingi yake!”
8Ee Babuloni, utaangamizwa!
Heri yule atakayekulipiza mabaya uliyotutenda!
9Heri yule atakayewatwaa watoto wako
na kuwapondaponda mwambani!