Zaburi 87

Zaburi 87

Sifa ya Yerusalemu

1Mungu amejenga mji wake

juu ya mlima wake mtakatifu.

2Mwenyezi-Mungu anaupenda mji wa Siyoni,

kuliko makao mengine ya Yakobo.

3Mambo ya fahari yanasemwa juu yako, ee mji wa Mungu:[#87:1-3 Yahusu mahali ambapo hekalu lilikuwa limejengwa.]

4“Miongoni mwa wale wanijuao mimi,

wapo watu wa Misri na Babuloni.

Kadhalika Filistia, Tiro na Kushi,

wote walizaliwa kwako!”

5Na kuhusu Siyoni itasemwa:

“Siyoni ni mama wa huyu na huyu;

Mungu Mkuu atauthibitisha.”

6Mwenyezi-Mungu ataandika katika kitabu,

atakapoorodhesha watu:

“Huyu amezaliwa huko!”

7Wote wanacheza ngoma na kuimba:

“Siyoni, chanzo chetu ni kwako.”

Copyright The Bible Society of Tanzania, 1993 The Bible Society of Kenya 1993
Published by: Bible Society of Tanzania