The chat will start when you send the first message.
1Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
2Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
Kutoka wazao wa Yuda:
7Kutoka wazao wa Benyamini:
10Kutoka makuhani:
15Kutoka Walawi:
19Mabawabu:
20Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
21Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
22Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
23Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
24Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
25Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyouzunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
26katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
27katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
28katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
29katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
30Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba hadi Bonde la Hinomu.
31Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
32katika Anathothi, Nobu na Anania,
33katika Hazori, Rama na Gitaimu,
34katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
35katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
36Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.