Zaburi 126

Zaburi 126

Zaburi 126

Kurejeshwa kutoka uhamisho

1Mwenyezi Mungu alipowarejesha mateka Sayuni,

tulikuwa kama watu walioota ndoto.

2Vinywa vyetu vilijaa kicheko,

ndimi zetu zilijaa nyimbo za shangwe.

Ndipo iliposemwa miongoni mwa mataifa,

“Mwenyezi Mungu amewatendea mambo makuu.”

3Mwenyezi Mungu ametutendea mambo makuu,

nasi tumejaa furaha.

4Ee Mwenyezi Mungu, turejeshee watu wetu waliotekwa,

kama vijito katika Negebu.

5Wapandao kwa machozi

watavuna kwa nyimbo za shangwe.

6Yeye azichukuaye mbegu zake

kwenda kupanda, huku akilia,

atarudi kwa nyimbo za shangwe,

akichukua miganda ya mavuno yake.

Neno: Maandiko Matakatifu™ NMM™ Hakimiliki © 2018, 2024 na Biblica, Inc. Imetumiwa kwa ruhusa. Haki zote zimehifadhiwa duniani kote. Kiswahili Contemporary Scriptures™ Copyright © 2018, 2024 by Biblica, Inc. Used with permission. All rights reserved worldwide.
Published by: Biblica, Inc.