Zaburi 150

Zaburi 150

Sifa kwa ukuu Mwingi wa Mungu

1Haleluya.

Msifuni Mungu katika patakatifu pake;

Msifuni katika anga la uweza wake.

2Msifuni kwa matendo yake makuu;

Msifuni kwa kadiri ya wingi wa ukuu wake.

3Msifuni kwa mvumo wa baragumu;

Msifuni kwa kinanda na kinubi;

4Msifuni kwa matari na kucheza;[#Kut 15:20; Isa 38:20]

Msifuni kwa zeze na filimbi;

5Msifuni kwa matoazi yaliayo;

Msifuni kwa matoazi yavumayo sana.

6Kila mwenye pumzi na amsifu BWANA.[#Ufu 5:13]

Haleluya.

The Holy Bible in Kiswahili, Revised Union Version © Bible Society of Tanzania and Bible Society of Kenya, 2013. 
Published by: Bible Society of Tanzania