The chat will start when you send the first message.
1Mungu, unihifadhi mimi,[#Zab 25:20]
Kwa maana nakukimbilia Wewe.
2Nimemwambia BWANA, Ndiwe BWANA wangu;
Sina wema ila utokao kwako.
3Nao watakatifu waliopo duniani, ndio Walio bora,
Hao ndio niliopendezwa nao.
4Huzuni zao zitaongezeka
Wambadilio Mungu kwa mwingine;
Sitazimimina sadaka zao za damu,
Wala kuyataja majina yao midomoni mwangu.
5BWANA ndiye fungu la posho langu,
Na la kikombe changu;
Wewe unayaamua maisha yangu.
6Mipaka yangu imeangukia mahali pema,
Naam, nimepata urithi mzuri.
7Nitamhimidi BWANA aniongozaye,
Wakati wa usiku pia moyo wangu hunishauri.
8Nimemweka BWANA mbele yangu daima,[#Mdo 2:25-28]
Kwa kuwa yuko kuliani mwangu, sitaondoshwa.
9Kwa hiyo moyo wangu unafurahi,
Nayo nafsi yangu inashangilia,
Naam, mwili wangu nao utakaa kwa kutumaini.
10Maana hutaitupa kuzimu nafsi yangu,[#Mdo 13:35; Zab 49:15; Mdo 2:27; Dan 9:24; Lk 1:35]
Wala hutamtoa mtakatifu wako aone uharibifu.
11Utanijulisha njia ya uzima;[#Mdo 2:28]
Mbele za uso wako kuna furaha tele;
Na katika mkono wako wa kulia
Mna mema ya milele.