Zaburi 15

Zaburi 15

Rafiki ya Mungu

1Nani ee Mwenyezi-Mungu atakayekaa hemani mwako?

Nani atakayeishi juu ya mlima wako mtakatifu?

2Ni mtu aishiye bila lawama,

atendaye daima yaliyo mema,

asemaye ukweli kutoka moyoni;

3ni mtu asiyesengenya watu,

asiyemtendea uovu rafiki yake,

wala kumfitini jirani yake;

4ni mtu anayewadharau wafisadi,

lakini huwaheshimu wamchao Mwenyezi-Mungu;

ni mtu asiyegeuza kiapo chake hata kikimtia hasara;

5asiyekopesha fedha yake kwa riba,

wala kupokea rushwa kumdhulumu asiye na hatia.

Mtu atendaye hayo,

kamwe hatatikisika.

Swahili Common Language DC Bible: Biblia Habari Njema kwa Watu Wote (Yenye Vitabu vya Deuterokanoni): Tafsiri ya Ushirikiano wa Makanisa (BHN): Hakimiliki © Chama cha Biblia cha Tanzania na Chama cha Biblia cha Kenya, 1995, 2001. Haki zote zimehifadhiwa.  
Published by: Bible Society of Tanzania